THE INSTITUTE OF FINANCE MANAGEMENT
IFM ALUMNI COMMUNITY

IFMSO WAKABIDHI VISIMA VIWILI HOSPITALI YA WILAYA YA BAGAMOYO, MKOANI PWANI.

Picha ya pamoja baada ya viongozi wa umoja wa wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha “The Institute of Finance Management Students’ Organisation – IFMSO”, kukabidhi visima viwili vya maji kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bagamoyo, Bw. Majid Mhina (wa kwanza kushoto). Visima hivi vilikabidhiwa kwa viongozi wa Hospitali ya Wilaya ya Bagamoyo tarehe 13 Aprili 2024, ikiwa kama sehemu ya kutoa misaada kwa jamii na kuchangia maendeleo ya nchi kwa ujumla. Viongozi mbalimbali walishuhudia tukio hili (kuendelea kutoka kushoto: Dkt Michael N Sam, Afisa Habari wa Chuo; Bw Hamisi Kihongoa, Mshauri wa wanafunzi; Bi Mwanaharusi Hamisi Jarufu, Diwani wa Kata ya Magomeni, Halmashauri Bagamoyo; Dkt Luiana Lyimo, mwakilishi wa Mganga Mkuu wa Wilaya, Dkt Shabani Ngole, mwakilishi wa Mkuu wa Chuo; Bw Sweetbert Macha, Mwenyekiti wa Kamati ya Matendo ya Hisani; na Bw Jerome Zachariah, Katibu wa Kamati ya Matendo ya Hisani). 

Contacts

P.O Box 3918, 5 Shaaban Robert Street

11101 Dar es salaam

+255 22 2112931-4

Fax : +255 22 2112935

alumni@ifm.ac.tz | +255222112931-4

Quick Links
Undergraduate Programmes
Postgraduate Programmes
Fee Structure
Frequently Asked Questions
Research Areas
Customers Service Delivery Charter
© 2024 The Institute of Finance Management. All rights reserved.