THE INSTITUTE OF FINANCE MANAGEMENT
IFM ALUMNI COMMUNITY

MAFUNZO YA UTAWALA BORA NA UADILIFU KWA WAJUMBE WA KAMATI MBALIMBALI

“Ni muhimu sana kuwa makini kwenye uadilifu, maana huu ni msingi mkuu wa utumishi wa umma”. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha, Prof Josephat Lotto (Picha ya Chini; katikati – mstari wa waliokaa), Tarehe 24 Mei 2024, alipokuwa akifungua mafunzo ya Utawala Bora na Uadilifu kwa Wajumbe wa Kamati Maalumu ya Menejimenti. Aliongezea kuwa, “uadilifu ndiyo nguzo muhimu katika kuimarisha uwazi na uwajibikaji”. Mafunzo hayo yamefanyika kwa siku tatu, tarehe 22 – 24 Mei 2024, katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha. Mafunzo ya Utawala Bora na Uadilifu yalitolewa kwa Maafisa Mrejesho na Wajumbe wa Kamati ya Uadilifu (Picha ya Juu), na kwa Wajumbe wa Kamati Maalumu ya Menejimenti (Picha ya Chini). Mafunzo hayo yalitolewa na wawezeshaji kutoka Ofisi ya Raisi – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, na kutoka Ofisi ya Raisi – Ikulu. Lengo lilikuwa ni kuongeza uelewa kuhusu utawala bora kwa wajumbe wa kamati hizo.

Contacts

P.O Box 3918, 5 Shaaban Robert Street

11101 Dar es salaam

+255 22 2112931-4

Fax : +255 22 2112935

alumni@ifm.ac.tz | +255222112931-4

Quick Links
Undergraduate Programmes
Postgraduate Programmes
Fee Structure
Frequently Asked Questions
Research Areas
Customers Service Delivery Charter
© 2025 The Institute of Finance Management. All rights reserved.